NAMNA YA KUTENGENEZA PESA KUTOKA GOOGLE NA SIMU YAKO


Kama una nia au lengo la kuanza kujitengenezea pesa kutoka youtube au google na una mbinu kidogo au hujui kabisa mahali pakuanzia basi leo umepata kitu kitakachokusaidia kutimiza lengo hilo. Kuna mambo machache sana ya kuzingatia ili kuweza kufanikisha jambo hili ukiachana na ule utalamu au ujuzi wa kutumia mtandao kwa maana ya internet fauatayo ni muhimu zaidi kuyafahamu:

Youtube ni bidhaa ya google. Amini kuwa unaweza kutengeneza pesa youtube kwa sababu watu wengine pia wanafanya hivyo. Unaweza kutengeneza pesa kutoka google bila hata kuitumia youtube. Google Adsense (Hii ndio hutoa kibali cha wewe kupata pesa)

Google ni kampuni kubwa ambayo ina huduma nyingi ikiwepo hii ya youtube na zingine nyingi zinazoweza kukufanya utengeneze pesa endapo utaweza kuzifahamu na kuzitumia kwa lengo hilo; hivyo youtube ukiitumia kama moja ya huduma za google unaweza kuingiz pesa kubwa sana.

NAMNA YA KUPATA PESA KUTOKA YOUTUBE
Ili uweze kupata pesa kutoka youtube itakubidi kuyafahamu na kuyafanya haya yafuatayo ni marahisi sana kama una nia na baada ya muda kidogo unaweza kuwa shuhuda wa watu wengine au kuwaelekeza pia.
  1. ·         Fungua email ya google kwa maana ya www.gmail.com ili upate nafasi ya kuweza kujisajili Youtube
  2.      Baaada ya kufungua email hio fungua youtube channel kwa kutumia email yako hio hapo juu na channel yako unaweza kuipa jina lolote unalotaka; kwa mfano, HELA TIME, MTONYO DAY nakadhalika.
  3.     Anza kuweka vitu kwenye channel yako hio na kuwashirikisha watu wavione. Vitu hivi vinaweza kuwa video au audio (sauti) zinazoelezea au kusikika kuhusu kitu fulani

BAADA YA HAPO HAYA YATAFATA
Baada ya kuendelea kutoa vitu vyako na watu wakavipenda watajiunga na channel yako kwa maana ya kusubscribe ili kila utakapoweka vitu wavione bila kuwambia na utakuwa unaona namba ya watu au wafuatiliaji wako inaongezeka kwe nye sehemu ya subscribers. Ukisha fikisha idadi ya wafuasi (subscribers) kuanzia elfu moja (1000) utaomba kuunganishwa na kitu kinachoitwa Google Adsense ili uanze kulipwa pesa kulingana na watu wanaotembelea na kuangalia vitu kwenye channel yako. Lakini lazima hao subscribers wapatikane ndani ya kipindi kisichozidi mwaka mmoja tangu umefungua channel yako youtube, ukizidisha mwaka hujafanikiwa kuwapata hoa 1000 hutoweza kupata Adense na kwa maana hio hutoweza kupata pesa. Hii nayo utatumia email yako ile uliyofungua kupitia www.gmail.com.

Baada ya kuomba kuunganishwa na hii adsense na kupata ndani siku kadhaa utafanya settings kwa maana ya mfumo wa nama ya kuonesha matangazo kwenye channel yako ili upate pesa kwa sababu lengo kuu la kuomba adsense ni kuwaomba google wapitishe matangazo yao kwenye channel yako ili watu wako wayaone na ulipwe pesa.
Baada ya kumaliza hilo utaenda kwenye akaunti yako ya google adesense kuweka njia ya wewe kupokea malipo kwa maana ya akaunti ya banki. Na hapo utabakia kuendelea kuweka vitu kama kawaida watu wanavyopenda kuona au kusikiliza na kujipatia pesa.

KUTENGENEZA PESA KUTOKA GOOGLE BILA HATA KUITUMIA YOUTUBE
Hii ni njia mabayo unaweza kuachana na youtube kabisa ila bado utahitaji kitu muhimu sana kinaitwa Google Adsense kulifanikisha hili pia. Hapa ni kwa wale wanotumia blogs, website na Apps za simu kufikisha vitu vyao kwa watu.
Haya ni ya muhimu sana kuyafahamu ili kuweza kupata pesa kutoka google kupitia blogs na website.
·         Blogger na Blog
Kama niivyosema mwanzo kuwa google wana huduma nyingi sana pia hizi ni zao; blogger na blog ambazo husaidia mtu kufungua blog yake au website kwa kutumia email yake na kuanza kuchapisha makala ambayo watu watayasoma na yeye akalipwa. Makala haya yanaweza kuwa katika mtindo wa maandishi, sauti (audio), picha na video. Kwa lugha yoyote ile duniani.
Hawa nao wanaotumia njia hii wataomba kuunganishwa na google adsense ili walipwe pesa kama ilivyo kwa youtube kwa sababu pia nao wataonesha matangazo ya google kwenye website na blog zao.
Haya yote ni kwa utaratibu unaotumiwa na google kwa kipindi hiki mwaka huu wa 2018 japo zamani haikuwa hivi kwa maana ilikuwa rahisi zaidi hasa youtube.
Yapo mengi kuhusu jambo hili ambalo mtu yeyote anaweza kulifanya na kujipatia pesa kutoka google na huduma zao ila kwa sasa tunaishia hapa nadhani umepata mwanga kidogo au umefahamu ulilokuwa hujui. Hivyo basi kama unadhani kuna swali au unahitaji msaada basi:
 wasilina nasi kwa simu namba 0743536577 au email: gericml@gmail.com



NAMNA YA KUTENGENEZA PESA KUTOKA GOOGLE NA SIMU YAKO NAMNA YA KUTENGENEZA PESA KUTOKA GOOGLE NA SIMU YAKO Reviewed by Geric Media Live on September 20, 2018 Rating: 5

No comments:

Powered by Blogger.